Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL-PESA Bw. Richard Mayongela akiongozana na Wajumbe wengine wametembelea Banda la Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), ambapo walijionea huduma mbalimbali za kidijitali na suluhisho za kifedha zinazotolewa kupitia T-PESA kwa wananchi, taasisi na wafanyabiashara.
Maafisa wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) wanaendelea kuwahudumia wananchi wanaotembelea Banda la TTCL katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), kwa kuwapatia elimu kuhusu huduma na suluhisho mbalimbali za mawasiliano na teknolojia za kidijitali zinazotolewa na TTCL.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) Moremi Marwa, ametembelea mabanda ya taasisi mbalimbali zinazoshiriki Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), kwa lengo la kujionea ubunifu wa teknolojia, kuimarisha ushirikiano wa kimkakati na kutambua fursa zinazoweza kuchochea maendeleo ya uchumi wa kidijitali nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) Moremi Marwa amewaalika wananchi kutembelea Banda la TTCL katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) ili kujionea mageuzi ya kiteknolojia na suluhisho mbalimbali za kidijitali zinazotolewa na Shirika katika kuimarisha huduma za mawasiliano na kuchochea uchumi wa kidijitali nchini.
Balozi wa Jamhuri ya Angola nchini Tanzania, Mheshimiwa Domingos Coelho, ametembelea Banda la Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius K. Nyerere.
Baadhi ya Viongozi wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) wametembelea banda la TTCL katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limepokea wanafunzi wa Shule ya Sekondari St. Therese Mapinga waliotembelea makao Makuu ya shirika kwa ziara ya mafunzo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa utafiti wao wa kitaaluma (Project Work) wenye mada isemayo, "The Role of TTCL Corporation in Improving Communication in Tanzania."
WAZIRI wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga, ameipongeza Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) kwa kuendelea kufanya vizuri kibiashara, kupata faida, kutoa gawio kwa Serikali pamoja na kutunukiwa tuzo maalum na Rais Samia Suluhu Hassan.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kutekeleza mkakati wake wa kuboresha mazingira ya kazi kwa kukabidhi magari sita (6) mapya yenye thamani ya Shilingi milioni 903 kwa Meneja wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, Meneja wa Network Operations and Maintenance pamoja na Meneja wa Network Planning, hatua inayolenga kuongeza ufanisi wa shughuli za kiutendaji na utoaji wa huduma kwa wananchi.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limetunukiwa tuzo ya kutambua mchango wake mkubwa katika kufanikisha Kongamano la Kwanza la Mwaka la Ulinzi wa Taarifa Binafsi na Faragha, baada ya kudhamini huduma ya intaneti ya uhakika iliyowezesha shughuli zote za kongamano hilo kufanyika kwa ufanisi.
TTCL tunamshukuru Naibu Gavana wa Benki Kuu kwa kutembelea banda letu na kwa kutambua mchango wa Shirika katika kujenga Tanzania ya kidijitali.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) linaendelea kutumia Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) kutoa huduma na elimu kwa wananchi kuhusu bidhaa na huduma mbalimbali za mawasiliano zinazotolewa na Shirika hilo.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeandika historia mpya baada ya kutunukiwa Tuzo Maalum na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia mafanikio ya kurejea kwenye faida kwa mara ya kwanza baada ya kipindi kirefu cha changamoto za kifedha.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limejipanga kikamilifu kuhakikisha wateja na wananchi wanaotembelea Banda Na. 26 katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) wanapata huduma bora, elimu kuhusu bidhaa na huduma mbalimbali za kidijitali, pamoja na suluhisho zinazokidhi mahitaji yao.
Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Dkt. Switbert Zacharia Mkama (Mb), amefungua rasmi Kongamano la Kwanza la Kitaifa la Faragha na Ulinzi wa Taarifa Binafsi 2026, linalofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam, kuanzia Juni 29 hadi Julai 1, 2026.