info@ttcl.co.tz
+255 22 210 0100

Latest From Our Blog

News
July 7, 2026 13:29:31 | By Ester Mbanguka VIONGOZI WA BODI YA T-PESA WATEMBELEA BANDA LA TTCL SABASABA 2026

Mwenyekiti wa Bodi ya TTCL-PESA Bw. Richard Mayongela akiongozana na Wajumbe wengine wametembelea Banda la Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), ambapo walijionea huduma mbalimbali za kidijitali na suluhisho za kifedha zinazotolewa kupitia T-PESA kwa wananchi, taasisi na wafanyabiashara.

News
July 6, 2026 22:34:07 | By Ester Mbanguka WANANCHI WAENDELEA KUNUFAIKA NA OFA ZA TTCL SABASABA 2026

Maafisa wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) wanaendelea kuwahudumia wananchi wanaotembelea Banda la TTCL katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), kwa kuwapatia elimu kuhusu huduma na suluhisho mbalimbali za mawasiliano na teknolojia za kidijitali zinazotolewa na TTCL.

News
July 6, 2026 17:42:31 | By Ester Mbanguka MKURUGENZI MKUU TTCL ATEMBELEA MABANDA YA TAASISI ZA MBALIMBALI SABASABA 2026

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) Moremi Marwa, ametembelea mabanda ya taasisi mbalimbali zinazoshiriki Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), kwa lengo la kujionea ubunifu wa teknolojia, kuimarisha ushirikiano wa kimkakati na kutambua fursa zinazoweza kuchochea maendeleo ya uchumi wa kidijitali nchini.

News
July 4, 2026 19:36:11 | By Ester Mbanguka MKURUGENZI MKUU TTCL AWAKARIBISHA WANANCHI KUJIONEA SULUHISHO ZA KIDIJITALI SABASABA 2026

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) Moremi Marwa amewaalika wananchi kutembelea Banda la TTCL katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) ili kujionea mageuzi ya kiteknolojia na suluhisho mbalimbali za kidijitali zinazotolewa na Shirika katika kuimarisha huduma za mawasiliano na kuchochea uchumi wa kidijitali nchini.

News
July 4, 2026 19:32:05 | By Ester Mbanguka BALOZI WA ANGOLA NCHINI TANZANIA ATEMBELEA BANDA LA TTCL SABASABA 2026

Balozi wa Jamhuri ya Angola nchini Tanzania, Mheshimiwa Domingos Coelho, ametembelea Banda la Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius K. Nyerere.

News
July 3, 2026 22:50:14 | By Ester Mbanguka VIONGOZI WA TTCL WATEMBELEA BANDA LA TTCL SABASABA 2026, WASISITIZA HUDUMA BORA KWA WATEJA

Baadhi ya Viongozi wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) wametembelea banda la TTCL katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.

Live from Mount Kilimanjaro