info@ttcl.co.tz
+255 22 210 0100

Latest From Our Blog

News
June 23, 2026 10:28:50 | By Ester Mbanguka TTCL YAPONGEZWA KWA KUUNGA MKONO AJENDA YA TANZANIA YA KIDIJITALI

Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI (Afya), Mhe. Dkt. Jafar Rajab Seif, amelipongeza Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) kwa mchango wake katika kuimarisha miundombinu ya mawasiliano na kuunga mkono jitihada za Serikali za kujenga uchumi wa kidijitali kupitia utoaji wa huduma za kisasa za TEHAMA.

News
June 23, 2026 10:24:03 | By Ester Mbanguka MHE. HALIMA DENDEGO AHAMASISHA MATUMIZI YA HUDUMA ZA TTCL

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego, amewahimiza wananchi, taasisi za umma na binafsi pamoja na wafanyabiashara kuendelea kutumia huduma zinazotolewa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), akieleza kuwa Shirika hilo lina mchango mkubwa katika kuimarisha sekta ya mawasiliano na kuharakisha maendeleo ya uchumi wa kidijitali nchini.

News
June 17, 2026 17:26:40 | By Ester Mbanguka WATUMISHI WAHIMIZWA KUIMARISHA UWAJIBIKAJI KWA HUDUMA ENDELEVU KWA WANANCHI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Jakaya Kikwete (Mb), amezindua rasmi Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma, huku akiwataka watumishi wa umma nchini kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa weledi, uwajibikaji na kujituma katika kutoa huduma bora na endelevu kwa wananchi.

News
June 16, 2026 17:14:06 | By Ester Mbanguka TTCL YASHIRIKI MAONESHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA 2026 DODOMA

Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) linashiriki katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 yanayofanyika kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni 2026 katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.

News
June 11, 2026 17:38:11 | By Ester Mbanguka MKURUGENZI MKUU WA TTCL AKAGUA MIUNDOMBINU YA MAWASILIANO NA MIRADI YA UPANUZI WA FAIBA PEMBA

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Moremi Marwa, amefanya ziara ya kukagua miundombinu mbalimbali ya mawasiliano katika Mkoa wa Pemba ikiwa ni sehemu ya jitihada za Shirika za kuhakikisha uwekezaji uliofanywa katika sekta ya mawasiliano unaleta tija, unaimarisha huduma kwa wananchi na kuchochea ukuaji wa uchumi wa kidijitali.

News
June 11, 2026 17:32:18 | By Ester Mbanguka TTCL YAONGEZA KASI YA UPANUZI WA HUDUMA ZA FAIBA ARUSHA, MKURUGENZI MKUU AKAGUA MAENDELEO

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Moremi Marwa, amefanya ziara ya kukagua maendeleo ya utoaji wa huduma ya intaneti yenye kasi ya TTCL Faiba katika makazi ya wananchi jijini Arusha, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Shirika za kuhakikisha Watanzania wanapata huduma bora, za uhakika na zenye kukidhi mahitaji ya uchumi wa kidijitali.

Live from Mount Kilimanjaro