info@ttcl.co.tz
+255 22 210 0100

Latest From Our Blog

News
July 4, 2026 19:36:11 | By Ester Mbanguka MKURUGENZI MKUU TTCL AWAKARIBISHA WANANCHI KUJIONEA SULUHISHO ZA KIDIJITALI SABASABA 2026

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) Moremi Marwa amewaalika wananchi kutembelea Banda la TTCL katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) ili kujionea mageuzi ya kiteknolojia na suluhisho mbalimbali za kidijitali zinazotolewa na Shirika katika kuimarisha huduma za mawasiliano na kuchochea uchumi wa kidijitali nchini.

News
July 4, 2026 19:32:05 | By Ester Mbanguka BALOZI WA ANGOLA NCHINI TANZANIA ATEMBELEA BANDA LA TTCL SABASABA 2026

Balozi wa Jamhuri ya Angola nchini Tanzania, Mheshimiwa Domingos Coelho, ametembelea Banda la Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026), yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius K. Nyerere.

News
July 3, 2026 22:50:14 | By Ester Mbanguka VIONGOZI WA TTCL WATEMBELEA BANDA LA TTCL SABASABA 2026, WASISITIZA HUDUMA BORA KWA WATEJA

Baadhi ya Viongozi wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) wametembelea banda la TTCL katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.

News
July 3, 2026 16:05:13 | By Ester Mbanguka TTCL YAPOKEA WANAFUNZI WA ST. THERESE MAPINGA KWA ZIARA YA KIMAFUNZO

Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limepokea wanafunzi wa Shule ya Sekondari St. Therese Mapinga waliotembelea makao Makuu ya shirika kwa ziara ya mafunzo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa utafiti wao wa kitaaluma (Project Work) wenye mada isemayo, "The Role of TTCL Corporation in Improving Communication in Tanzania."

News
July 3, 2026 14:17:34 | By Ester Mbanguka WAZIRI KAPINGA AIPONGEZA TTCL KWA FAIDA NA GAWIO KWA SERIKALI

WAZIRI wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga, ameipongeza Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) kwa kuendelea kufanya vizuri kibiashara, kupata faida, kutoa gawio kwa Serikali pamoja na kutunukiwa tuzo maalum na Rais Samia Suluhu Hassan.

News
July 2, 2026 18:00:29 | By Ester Mbanguka TTCL YAENDELEA KUWEKEZA KATIKA VITENDEA KAZI, YAKABIDHI MAGARI SITA

Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kutekeleza mkakati wake wa kuboresha mazingira ya kazi kwa kukabidhi magari sita (6) mapya yenye thamani ya Shilingi milioni 903 kwa Meneja wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, Meneja wa Network Operations and Maintenance pamoja na Meneja wa Network Planning, hatua inayolenga kuongeza ufanisi wa shughuli za kiutendaji na utoaji wa huduma kwa wananchi.

Live from Mount Kilimanjaro