info@ttcl.co.tz
+255 22 210 0100

Latest From Our Blog

Sports
August 31, 2026 08:01:46 | By Debora Ngalima TTCL CHACHU YA MAPINDUZI YA KIDIJITALI KATIKA SOKA ZANZIBAR

Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Mhe. Dkt. Riziki Pembe Juma, amesema ushirikiano kati ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) na Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFF) una fursa kubwa ya kubadilisha uendeshaji wa soka Zanzibar kwa kutumia teknolojia za kidijitali.

News
August 29, 2026 21:22:12 | By Debora Ngalima TTCL YATOA MAFUNZO YA HUDUMA BORA KWA MTEJA KWA TIMU YA MAFUNDI WA FAIBA MKOANI DODOMA

Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), kupitia Kitengo cha Uhusiano kwa Umma kutoka Makao Makuu, kwa kushirikiana na watumishi wa TTCL Mkoa wa Dodoma pamoja na kampuni ya Huawei, limefanikisha mafunzo maalum ya huduma bora kwa mteja yaliyolenga timu ya mafundi wanaotoa huduma ya uunganishaji wa intaneti ya Faiba Kwa wateja mbalimbali wa TTCL.

News
August 28, 2026 08:06:35 | By Debora Ngalima POLISI DAR ES SALAAM YAWAKAMATA 11 KWA TUHUMA ZA HUJUMA MIUNDOMBINU YA TTCL

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limewakamata watu 11 wanaodaiwa kujihusisha na wizi, uharibifu, usafirishaji na biashara ya miundombinu ya mawasiliano ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), huku likisema hali ya usalama jijini kwa ujumla ni shwari.

Sports
August 24, 2026 23:28:05 | By Debora Ngalima T-PESA WADHAMINI NGAO YA JAMII 2026 ZANZIBAR

Kampuni Tanzu ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), T-PESA, kupitia huduma yake ya N-card, imeendelea kudhihirisha dhamira yake ya kuunga mkono maendeleo ya soka Zanzibar kwa kudhamini na kushiriki kikamilifu katika Mchezo wa Ngao ya Jamii 2026 uliozikutanisha KVZ FC na KMKM SC uliofanyika tarehe 23 Agosti 2026 katika Uwanja wa Mao, Zanzibar.

Sports
August 24, 2026 23:18:23 | By Debora Ngalima TTCL YASHIRIKI TAMASHA LA KIJA 2026

Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kushiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii kwa kushirikiana na wadau, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha uhusiano na jamii, kuhamasisha matumizi ya teknolojia katika maisha ya kila siku. ‎Katika kuunga mkono juhudi hizo, TTCL imeshiriki Tamasha la Kinondoni Jogging Association (KIJA) 2026, lililofanyika Viwanja Vya Posta Kijitonyama likilenga kuwakutanisha wananchi katika shughuli za kijamii, afya na burudani. ‎

News
August 21, 2026 19:07:11 | By Debora Ngalima TTCL YAZINDUA FAIBA MLANGONI KWAKO AWAMU YA PILI, WATEJA 400,000 KUNUFAIKA

Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limezindua rasmi utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Mradi wa Faiba Mlangoni Kwako (FTTH), hatua inayolenga kuongeza upatikanaji wa huduma ya intaneti ya kasi kwa wananchi, taasisi za umma na binafsi pamoja na wafanyabiashara kupitia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano. Uzinduzi wa mradi huo umefanyika leo, Agosti 21, 2026, katika Hoteli ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam, ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki (Mb).

Live from Mount Kilimanjaro