Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kuunga mkono juhudi za Serikali za kujenga mazingira wezeshi kwa uchumi wa kidijitali Zanzibar kwa kuwezesha huduma ya intaneti katika mradi wa makazi wa Amani Residency, uliopo Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, kupitia huduma yake ya Faiba Mlangoni Kwako.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limetajwa kuwa kinara katika utoaji wa huduma bora za mawasiliano nchini, hatua inayothibitisha mafanikio ya uwekezaji wa muda mrefu katika miundombinu na mifumo ya huduma kwa wateja.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemkabidhi cheti Meneja TTC Zanzibar Bi. Nasra Mugheiry , ishara ya kutambua mchango wa Shirika la Mawasiliano (TTCL) katika kudhamini, kushiriki na kuunga mkono Tamasha la Kizimkazi ambalo lilifikia kilele Agosti 14, 2026 Kizimkazi, Kusini Unguja, Zanzibar.
Tamasha la Kizimkazi 2026 limefikia kilele chake leo katika Viwanja vya Makunduchi, Zanzibar, likihudhuriwa na kufungwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewasalimia Viongozi na Wafanyakazi wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) waliokuwa wakiliwakilisha Shirika katika banda la maonesho wakati wa Tamasha la Kizimkazi 2026.
Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia na Mbunge wa Makunduchi, Mhe. Wanu Hafidh Ameir, ametembelea banda la Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) katika Maonesho ya Tamasha la Kizimkazi 2026, Zanzibar.