info@ttcl.co.tz
+255 22 210 0100

Latest From Our Blog

News
August 24, 2026 23:28:05 | By Debora Ngalima T-PESA WADHAMINI NGAO YA JAMII 2026 ZANZIBAR

Kampuni Tanzu ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), T-PESA, kupitia huduma yake ya N-card, imeendelea kudhihirisha dhamira yake ya kuunga mkono maendeleo ya soka Zanzibar kwa kudhamini na kushiriki kikamilifu katika Mchezo wa Ngao ya Jamii 2026 uliozikutanisha KVZ FC na KMKM SC uliofanyika tarehe 23 Agosti 2026 katika Uwanja wa Mao, Zanzibar.

News
August 24, 2026 23:18:23 | By Debora Ngalima TTCL YASHIRIKI TAMASHA LA KIJA 2026

Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kushiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii kwa kushirikiana na wadau, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha uhusiano na jamii, kuhamasisha matumizi ya teknolojia katika maisha ya kila siku. ‎Katika kuunga mkono juhudi hizo, TTCL imeshiriki Tamasha la Kinondoni Jogging Association (KIJA) 2026, lililofanyika Viwanja Vya Posta Kijitonyama likilenga kuwakutanisha wananchi katika shughuli za kijamii, afya na burudani. ‎

News
August 21, 2026 19:07:11 | By Debora Ngalima TTCL YAZINDUA FAIBA MLANGONI KWAKO AWAMU YA PILI, WATEJA 400,000 KUNUFAIKA

Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limezindua rasmi utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Mradi wa Faiba Mlangoni Kwako (FTTH), hatua inayolenga kuongeza upatikanaji wa huduma ya intaneti ya kasi kwa wananchi, taasisi za umma na binafsi pamoja na wafanyabiashara kupitia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano. Uzinduzi wa mradi huo umefanyika leo, Agosti 21, 2026, katika Hoteli ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam, ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki (Mb).

News
August 17, 2026 14:58:58 | By Debora Ngalima TTCL YAWEZESHA INTANETI YA KASI KATIKA MAKAZI YA AMANI RESIDENCY ZANZIBAR

Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kuunga mkono juhudi za Serikali za kujenga mazingira wezeshi kwa uchumi wa kidijitali Zanzibar kwa kuwezesha huduma ya intaneti katika mradi wa makazi wa Amani Residency, uliopo Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, kupitia huduma yake ya Faiba Mlangoni Kwako.

News
August 17, 2026 14:48:48 | By Debora Ngalima TTCL YAIBUKA KINARA WA HUDUMA BORA ZA MAWASILIANO NCHINI

Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limetajwa kuwa kinara katika utoaji wa huduma bora za mawasiliano nchini, hatua inayothibitisha mafanikio ya uwekezaji wa muda mrefu katika miundombinu na mifumo ya huduma kwa wateja.

News
August 17, 2026 14:42:45 | By Debora Ngalima TTCL YATUNUKIWA CHETI CHA SHUKRANI KIZIMKAZI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemkabidhi cheti Meneja TTC Zanzibar Bi. Nasra Mugheiry , ishara ya kutambua mchango wa Shirika la Mawasiliano (TTCL) katika kudhamini, kushiriki na kuunga mkono Tamasha la Kizimkazi ambalo lilifikia kilele Agosti 14, 2026 Kizimkazi, Kusini Unguja, Zanzibar.

Live from Mount Kilimanjaro