Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Kairuki, amewataka Watanzania kuchangamkia fursa zinazotokana na huduma za mawasiliano zinazotolewa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), hususan huduma za intaneti ya kasi kupitia Faiba Mlangoni Kwako, ili kuongeza matumizi ya teknolojia katika shughuli za kila siku na kuchangia ukuaji wa uchumi wa kidijitali nchini.
Mkuu wa Wilaya ya Longido, Mhe. Salum Abdalah Kalli, amelipongeza Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) kwa mchango wake katika kuimarisha sekta ya mawasiliano nchini na kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na za uhakika, ikiwemo huduma ya intaneti kupitia Faiba Mlangoni Kwako.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), kupitia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB), na Burundi Backbone System (BBS) wamesaini mkataba wa kuongeza uwezo wa huduma za mawasiliano nchini Burundi kutoka 4Gbps hadi 10Gbps.
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Mhe. Dkt. Riziki Pembe Juma, amesema ushirikiano kati ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) na Shirikisho la Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFF) una fursa kubwa ya kubadilisha uendeshaji wa soka Zanzibar kwa kutumia teknolojia za kidijitali.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), kupitia Kitengo cha Uhusiano kwa Umma kutoka Makao Makuu, kwa kushirikiana na watumishi wa TTCL Mkoa wa Dodoma pamoja na kampuni ya Huawei, limefanikisha mafunzo maalum ya huduma bora kwa mteja yaliyolenga timu ya mafundi wanaotoa huduma ya uunganishaji wa intaneti ya Faiba Kwa wateja mbalimbali wa TTCL.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limewakamata watu 11 wanaodaiwa kujihusisha na wizi, uharibifu, usafirishaji na biashara ya miundombinu ya mawasiliano ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), huku likisema hali ya usalama jijini kwa ujumla ni shwari.