Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limepokea wanafunzi wa Shule ya Sekondari St. Therese Mapinga waliotembelea makao Makuu ya shirika kwa ziara ya mafunzo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa utafiti wao wa kitaaluma (Project Work) wenye mada isemayo, "The Role of TTCL Corporation in Improving Communication in Tanzania."
WAZIRI wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith Kapinga, ameipongeza Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) kwa kuendelea kufanya vizuri kibiashara, kupata faida, kutoa gawio kwa Serikali pamoja na kutunukiwa tuzo maalum na Rais Samia Suluhu Hassan.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kutekeleza mkakati wake wa kuboresha mazingira ya kazi kwa kukabidhi magari sita (6) mapya yenye thamani ya Shilingi milioni 903 kwa Meneja wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, Meneja wa Network Operations and Maintenance pamoja na Meneja wa Network Planning, hatua inayolenga kuongeza ufanisi wa shughuli za kiutendaji na utoaji wa huduma kwa wananchi.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limetunukiwa tuzo ya kutambua mchango wake mkubwa katika kufanikisha Kongamano la Kwanza la Mwaka la Ulinzi wa Taarifa Binafsi na Faragha, baada ya kudhamini huduma ya intaneti ya uhakika iliyowezesha shughuli zote za kongamano hilo kufanyika kwa ufanisi.
TTCL tunamshukuru Naibu Gavana wa Benki Kuu kwa kutembelea banda letu na kwa kutambua mchango wa Shirika katika kujenga Tanzania ya kidijitali.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) linaendelea kutumia Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) kutoa huduma na elimu kwa wananchi kuhusu bidhaa na huduma mbalimbali za mawasiliano zinazotolewa na Shirika hilo.