info@ttcl.co.tz
+255 22 210 0100

Latest From Our Blog

News
August 21, 2026 19:07:11 | By Debora Ngalima TTCL YAZINDUA FAIBA MLANGONI KWAKO AWAMU YA PILI, WATEJA 400,000 KUNUFAIKA

Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limezindua rasmi utekelezaji wa Awamu ya Pili ya Mradi wa Faiba Mlangoni Kwako (FTTH), hatua inayolenga kuongeza upatikanaji wa huduma ya intaneti ya kasi kwa wananchi, taasisi za umma na binafsi pamoja na wafanyabiashara kupitia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano. Uzinduzi wa mradi huo umefanyika leo, Agosti 21, 2026, katika Hoteli ya Johari Rotana jijini Dar es Salaam, ambapo mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki (Mb).

News
August 17, 2026 14:58:58 | By Debora Ngalima TTCL YAWEZESHA INTANETI YA KASI KATIKA MAKAZI YA AMANI RESIDENCY ZANZIBAR

Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limeendelea kuunga mkono juhudi za Serikali za kujenga mazingira wezeshi kwa uchumi wa kidijitali Zanzibar kwa kuwezesha huduma ya intaneti katika mradi wa makazi wa Amani Residency, uliopo Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, kupitia huduma yake ya Faiba Mlangoni Kwako.

News
August 17, 2026 14:48:48 | By Debora Ngalima TTCL YAIBUKA KINARA WA HUDUMA BORA ZA MAWASILIANO NCHINI

Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limetajwa kuwa kinara katika utoaji wa huduma bora za mawasiliano nchini, hatua inayothibitisha mafanikio ya uwekezaji wa muda mrefu katika miundombinu na mifumo ya huduma kwa wateja.

News
August 17, 2026 14:42:45 | By Debora Ngalima TTCL YATUNUKIWA CHETI CHA SHUKRANI KIZIMKAZI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemkabidhi cheti Meneja TTC Zanzibar Bi. Nasra Mugheiry , ishara ya kutambua mchango wa Shirika la Mawasiliano (TTCL) katika kudhamini, kushiriki na kuunga mkono Tamasha la Kizimkazi ambalo lilifikia kilele Agosti 14, 2026 Kizimkazi, Kusini Unguja, Zanzibar.

News
August 14, 2026 16:30:38 | By Debora Ngalima KIZIMKAZI 2026 YAFIKIA KILELE LEO ZANZIBAR, MHE. RAIS AFUNGA RASMI

Tamasha la Kizimkazi 2026 limefikia kilele chake leo katika Viwanja vya Makunduchi, Zanzibar, likihudhuriwa na kufungwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

News
August 14, 2026 16:19:54 | By Debora Ngalima MHE. RAIS APITA BANDA LA TTCL, AWASALIMIA VIONGOZI NA WAFANYAKAZI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewasalimia Viongozi na Wafanyakazi wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) waliokuwa wakiliwakilisha Shirika katika banda la maonesho wakati wa Tamasha la Kizimkazi 2026.

Live from Mount Kilimanjaro