Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) limejipanga kikamilifu kuhakikisha wateja na wananchi wanaotembelea Banda Na. 26 katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) wanapata huduma bora, elimu kuhusu bidhaa na huduma mbalimbali za kidijitali, pamoja na suluhisho zinazokidhi mahitaji yao.
Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Dkt. Switbert Zacharia Mkama (Mb), amefungua rasmi Kongamano la Kwanza la Kitaifa la Faragha na Ulinzi wa Taarifa Binafsi 2026, linalofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam, kuanzia Juni 29 hadi Julai 1, 2026.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) linashiriki katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba 2026) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe Profesa Riziki Shemdoe ametoa rai kwa wananchi kutumia huduma zinazotolewa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) huku akipongeza juhudi za Shirika hilo katika kutekeleza dhamira ya Serikali ya kujenga Tanzania ya kidijitali na kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora na za uhakika za mawasiliano.
Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI (Afya), Mhe. Dkt. Jafar Rajab Seif, amelipongeza Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) kwa mchango wake katika kuimarisha miundombinu ya mawasiliano na kuunga mkono jitihada za Serikali za kujenga uchumi wa kidijitali kupitia utoaji wa huduma za kisasa za TEHAMA.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego, amewahimiza wananchi, taasisi za umma na binafsi pamoja na wafanyabiashara kuendelea kutumia huduma zinazotolewa na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), akieleza kuwa Shirika hilo lina mchango mkubwa katika kuimarisha sekta ya mawasiliano na kuharakisha maendeleo ya uchumi wa kidijitali nchini.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Jakaya Kikwete (Mb), amezindua rasmi Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 yanayofanyika katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma, huku akiwataka watumishi wa umma nchini kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa weledi, uwajibikaji na kujituma katika kutoa huduma bora na endelevu kwa wananchi.
Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) linashiriki katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma 2026 yanayofanyika kuanzia tarehe 16 hadi 23 Juni 2026 katika Viwanja vya Chinangali Park, jijini Dodoma.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Moremi Marwa, amefanya ziara ya kukagua miundombinu mbalimbali ya mawasiliano katika Mkoa wa Pemba ikiwa ni sehemu ya jitihada za Shirika za kuhakikisha uwekezaji uliofanywa katika sekta ya mawasiliano unaleta tija, unaimarisha huduma kwa wananchi na kuchochea ukuaji wa uchumi wa kidijitali.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Moremi Marwa, amefanya ziara ya kukagua maendeleo ya utoaji wa huduma ya intaneti yenye kasi ya TTCL Faiba katika makazi ya wananchi jijini Arusha, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Shirika za kuhakikisha Watanzania wanapata huduma bora, za uhakika na zenye kukidhi mahitaji ya uchumi wa kidijitali.
Ujumbe kutoka Kampuni ya Kusafirisha Umeme nchini Uganda (Uganda Electricity Transmission Company Limited - UETCL) umetembelea Kijitonyama FTTx Experience Centre na kupongeza juhudi za Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) katika kuwekeza kwenye miundombinu na suluhisho za kidijitali zinazochangia maendeleo ya sekta ya mawasiliano nchini Tanzania na ukanda wa Afrika Mashariki.
Wafanyakazi wa TTCL Mkoa wa Pwani, wakiongozwa na Meneja wa Mkoa, Bw. Abdulrahim Chotta, wametembelea Kijitonyama FTTx Experience Centre kwa lengo la kujifunza, kubadilishana uzoefu na kuongeza uelewa kuhusu teknolojia za kisasa za mawasiliano zinazotolewa na Shirika.
Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Dkt. Switbert Zacharia Mkama (Mb), amewasilisha taarifa mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti katika kikao kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma tarehe 13 Mei 2026.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan amewahimiza Wafanyakazi kufanya kazi kwa bidii, uaminifu na weledi mkubwa ili kuchochea ujenzi wa uchumi imara,maendeleo ya jamii kwa kuzingatia misingi ya Amani na Mshikamano.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Moremi Marwa, akabidhi rasmi magari tisa (9) na bajaji ishirini na nane (28) kwa Wakuu wa Idara na Vitengo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha utekelezaji wa majukumu ya Shirika na kuboresha utoaji wa huduma kwa wateja.