Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Mawasiliano la Tanzania- TTCL Bi. Zuhura Muro amesema TTCL inauwezo wa kuifanya Tanzania kuwa nchi kiongozi katika ukanda wa Afrika Mashariki na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC kutokana uwepo wa miundombinu bora ya mawasiliano yenye uwezo wa kufanikisha ukuaji wa uchumi wa kidjitali.
Tarehe 8 Machi kila mwaka ni Siku ya Kimataifa ya Wanawake, ama Siku ya Wanawake Duniani. Katika siku hii, wanawake wa Shirika la Mawasiliano Tanzania huungana na Wanawake wenzao duniani kote kuadhimisha siku hii muhimu.